CCM YAFAFANUA MFUMOKO WA BEI WA MAFUTA NCHI YAITAKA SERIKALI KUJENGA VITUO VYA GESI

Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa, Ndugu 𝗞𝗲𝗻𝗮𝗻𝗶 𝗞𝗶𝗵𝗼𝗻𝗴𝗼𝘀𝗶, ametoa maelekezo kwa serikali kuhakikisha ujenzi wa vituo vya kuchaji gesi asilia iliyoshindiliwa (CNG) kote nchini pamoja na ufungaji wa mfumo wa gesi kwenye magari yote ya serikali na vyombo vya usafiri wa umma, kuanza na Mikoa Yenye idadi kubwa ya watu.

Kihongosi ametoa maelekezo hayo kwa niaba ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wakati alipokuwa wakati akizungumza na waandishi wa Habari katika ukumbi wa White House uliopo Makao Makuu ya CCM Jijini Dodoma,  Aprili 7, 2026, Aidha  amebainisha mpango huo ni sehemu ya mkakati wa CCM wa kupunguza utegemezi wa mafuta na gharama za usafiri. “Hii itapunguza gharama za usafiri na pia kuokoa fedha za kigeni zinazotumika kuagiza mafuta,” alibainisha.

Aidha, amesisitiza ujenzi wa usafiri wa umma wa kisasa, ikiwemo vituo vya kuchaji vyombo vinavyotumia umeme, pamoja na miradi ya kiuchumi inayozalisha bidhaa za kuuza nje, ili kuimarisha uchumi wa ndani na kupungu

pia amebainisha kuwa Chama Cha Mapinduzi kimependekeza hatua nyingine za kudhibiti athari za ongezeko la bei ya mafuta duniani, ikiwemo kuanzisha Mfuko wa Kuhimili Ukali wa Bei za Mafuta, Hifadhi ya Mafuta ya Kimkakati, na Petroleum Hub itakayohakikisha upatikanaji wa mafuta kwa uhakika na kwa bei nafuu.

Aidha, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeitaka serikali kuanza mchakato wa kuhakikisha mafuta ya Petroli na dizeli yanaendelea kupatikana nchini pamoja na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania TPDC kuendelea kuwa kiungo muhimu katika uagizaji wa mafuta nchini kwa kudhibiti hujuma katika sekta ya mafuta hasa kwa njama za kutaka kuchepusha meli za mafuta na kwenda kuuza maeneo mengine.

Kihongosi amesistiza umuhimu wa kupunguza matumizi ya mafuta katika taasisi za serikali, binafsi na umma kwa ujumla, na kuhamasisha matumizi ya nishati mbadala. “Hii itatusaidia kuwa na uwezo wa kujiendesha kwa nishati mbadala pale changamoto za mafuta zinapotokea,” amesema Kihongosi 

Pia, amesema kuwa CCM  itaendelea kushirikiana na serikali kuhakikisha hatua zote zinazochukuliwa zinawalenga wananchi na kulinda maslahi mapana ya taifa.



No comments