UNGANISHAJI UMEME MOROGORO MBIONI KUANZA, REA YAKABIDHI ENEO
Wakandarasi wanaotekelza miradi ya kusambaza umeme nchini wametakiwa kushirikiana kwa karibu na Viongozi wa Serikali za Mitaa ili utekelezaji wa miradi ya kupeleka umeme kwa wananchi iweze kuleta tija na kuchochea uchumi wa nchi.
Hayo yamezungumzwa na Meneja wa Usimamizi wa Miradi ya Kusambaza Umeme kutoka Wakala wa Nishati Vijijini-REA, Deogratius Nagu katika kikao maalum cha kwanza cha kufungua mradi wa kuwaunganishia umeme wananchi mkoani Morogoro, ambacho kimehudhuriwa na Wataalam kutoka REA, TANESCO na Wakandarasi kampuni ya Magna Vis Group Ltd.
Katika hatua nyingine, Nagu ameeleza kuwa, mradi huo ni mahsusi katika kutekeleza mpango mkubwa wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kuongeza watumiaji wa umeme nchini.
Naye, Meneja wa TANESCO Mkoa wa Morogoro Kaskazini, Zawadi Macha, amesisitiza ubora wa mradi kuzingatiwa katika kipindi chote cha mradi na kuhakikisha wanawapa taarifa ya mradi mara kwa mara viongozi wa Serikali za Mitaa ili kuwawezesha kufahamu hatua mbalimbali za utekelezaji zinazofikiwa.
Takribani shilingi bilioni 6.6 zimetolewa na Serikali ili kuunganisha wateja wa awali wapatao 1,929 katika Mkoa wa Morogoro kuweza kupata huduma ya umeme na hatimaye kuwawesesha kuendesha shughuli zao za kiuchumi ikiwemo kuchomelea na machine za kusaga zinazotumia umeme.
Naye, Msimamizi wa mradi kutoka kampuni ya Magna Vis Group Ltd, James Kimaro, amesema watazingatia taratibu zote zilizopo katika mradi ili ziende sambamba katika kipindi chote cha utekelezani wa mradi huo mkoani Morogoro.


.jpeg)

Post a Comment