MECHI YA YANGA NA SILVER STRIKERS MASHABIKI KUSHUHUDIA BURE BENJAMINI MKAPA
Kikosi cha
Yanga kimeingia kambini kwa ajili ya kufanya maandilizi kueleka katika mchezo
wa klabu Bingwa Afrika dhidi ya Silver Strikers ya Malawi jumamosi wiki hii.
Meneja wa Habari
na mawasiliano Ally Kamweamesema kikosi
hicho kimeingia kambi leo mchana na kinaendelea na maandalizi yake huku
wapinzani wao wakitarajiwa kuwali nchini siku ya alhamisi sa mbili usiku.
Yanga inaingia
katika mchezo huo wa marejeano wakiwa nyuma kwa goli 1- 0 walipofuingwa ugenini
wikiendi iliyopita na kuiweka hatarini nafasi yao ya kufuzu hatua ya makundi
kama watashindwa kushinda zaidi ya goli moja wakiwa uwanja wa Benjamini mkapa.
Ally Kamwe
amesema amesikia maneno mengi yanaendelea kusema kwenye mitandao ya kijamii
kuhusu wachezaji lakini yote yatajibiwa kwa vitendo katika uwanja wa mchezo.
“Nimesoma
maneno mengi yanayoandikwa huko mitandaoni, wachezaji wetu wamesemwa sana na
niwaambie tu kuwa Yote tumeyasikia, wachezaji wetu wameyasikia yote na
wanayafanyia kazi, hatutawajibu kwa maneno, wengi waongea kwa Chuki na Roho
mbaya tu, wachezaji wetu watayajibu kwa vitendo yote yanayozungumzwa na
Inshaallah Jumamosi majibu yatapatikana.
“Tunajua
kuwa wanaotuombea mabaya siyo hao wamalawi, ni hawa hawa tunaoishi nao na kula
nao, wakati huu ndiyo wakati wa kuwajua dhahiri maadui zetu, niwaombe
wanayanga, raha ya Ngoma ucheze mdundo unaouona siyo unaousikia kwa watu,
twendeni kwa Mkapa tukaisapoti timu yetu na Inshaallah tutafuzu hatua ya
Makundi” Ally Kamwe
Amesema ombi
hili la kuweka mechi hii isiwe na viingilio lilikuwa gumu sana kukubaliwa
kwakuwa viongozi wetu wana mahitaji mengi sana ya kuiendesha timu yetu, lakini
kwa kutambua umuhimu wa mchezo huu iliulazimu Uongozi ukubali na kuweka kipaumbele
ushindi ambao kila mmoja wetu anauhitaji.
“Tumekubaliana
kuwa mechi hii imeondolewa viingilio majukwaa yote isipokuwa jukwaa la VIP A na
VIP B yamekuwa Reserved kwa waalikwa maalum ambao ni Wageni wetu pamoja na
wanachama wa Yanga wa Black Card.
Kuhusu
Kocha mpya, Ally amesema uongozi wa Yanga upo kwenye mchakato mzuri wa kumpata
kocha mpya na ndani ya siku tatu hizi mchakato huu utakuwa umekamilika, lakini mchezo
wa tarehe 25 utaongozwa na Care taker Patrick Mabedi.



Post a Comment