SHOMARI KAPOMBE KUWANIA TUZO YA CAF YA MCHEZAJI BORA KWA WACHEZAJI WA NDANI
Mchezaji wa
Simba raia wa Tanzania Beki wa kulia Shomari Kapombe ameingia kwenye Orodha ya
wachezaji kumi Bora wanaowania Tuzo za Caf za mwaka kwa wachezaji wa ndani.
Kapombe
anaingia kwenye Orodha hiyo akiwania Pamoja na wachezaji wengine kutoka vilabu
mbalimbali Afrika ikiwemo mabingwa wa ligi ya mabingwa Afrika Pyramid na
Mabingwa wa kombe la shirikisho la CAF Berkane ambao wametawala katika orodha
hiyo
Kapombe ni
Miongoni mwa wachezaji walioonesha kiwango bora msimu uliopita ambao amechangia
kwa kiasi kikubwa klabu yake ya Simba kufika katika hatua ya fainali ya
michuano ya kombe la shirikisho la Caf ambapo walipoteza dhidi ya Berkane.
Shomari
Kapombe ni mchezaji pekee anaetokea Tanzania na Afrika Mashariki aliyeingia
katika orodha hiyo.



Post a Comment