SIMBA YAIPANIA NSINGIZINI BENJAMINI MKAPA, WAJA NA "HATUJARIDHIKA TUNATAKA ZAIDI"
Kuelekea
katika mchezo wa marejeano wa klabu bingwa Afrika kati ya Simba na Nsingizini
ya Eswatini, Uongozi wa kalbu ya simba umesema bado haujarishika na matokeo ya
mchezo wa mkondo wa kwanza amabo walishinda 3 – 0 ugenini na wakitaka ushindi zaidi
katika mchezo ujao ambao utapigwa oktoba 26 katika uwanja wa benjamini Mkapa
jijini Dar es salaam
Simba wakuja
na kaulimbiu isemayo HATUJARIDHIKA, TUNATAKA ZAIDI ikiwa inalenga kutaka
kufahamu nini nini Mwalimu Pantev alimaanisha kusema hajaridhika baada ya
kumalizika kwa mchezo uliopita
Meneja wa Habari
na mawasiliano wa klabu ya Simba Ahmed Ally akizungumza na waandishi wa Habari leo
jijini Dar es salaam amesema kwenye mchezo wa kwanza mwalimu aliweka wazi
kwamba bado hajaridhika na kiwango cha timu yake, hivyo kipo kitu mwalimu
anakitaka na sisi bado hatujakijua.
"Mechi
ya Oktoba 26 itakuwa mechi ya kumuona Dimitar Pantev halisi akiwa na ukatili
kwenye uwanja wa vita na sisi tunakwenda na kaulimbiu ya HATUJARIDHIKA,
TUNATAKA ZAIDI.”
Aidha Ahmed
ally amesema kikosi chao kimerejesha hali nzuri ya uchezaji inafanya
mashambulizi muda wote na imekuwa simba ya kutisha na kusisitiza mashabiki kuwa
hawana sababu ya kukaa nyumbani simu ya mchezo huo.
"Tulikuwa
tunapiga kelele kwamba Simba yetu hatuelewi inavyocheza lakini sasa
imerejea, Simba ya kutisha imerejea,
Simba ya kushambulia muda wote imerejea sasa unabaki nyumbani kufanya nini. Na
haya sio maneno ya kutoka usingizi, haya ni maneno ya kuona inacheza na pale
mwalimu anasema uwanja ulikuwa mdogo. Sasa uwanja wa Mkapa anakwenda kwenye
uwanja mkubwa, njoo Uwanja wa Mkapa uone Simba ikifanya balaa zito."
"Msiba
pekee ndio hauna kiingilio, sisi tunakwenda kwenye starehe lazima kuwe na
kiingilio. Huwezi kwenda kumuona mchezaji wa Kombe la Dunia la Vilabu, Seleman
Mwalimu, Rushine, Kagoma, Morice, Nangu haiwezi kuwa bure. Siku hiyo sisi
tunakwenda kuenjoy, kama una babe wako njoo nae, kama una familia njoo nayo.
Hii ni starehe haiwezi kuwa bure."- Semaji Ahmed Ally.


Post a Comment