WIKI YA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA KUANZA KUADHIMISHA LEO NCHINI TANZANIA

Wiki ya magonjwa yasiyoambukiza (NCDs) nchini huadhimishwa wiki ya pili ya mwezi novemba kila mwaka. Kwa mwaka 2025 maadhimisho haya yanaadhimishwa kuanzia tarehe 10 hadi 15 kwa lengo la kuongeza uelewa wa umma kuhusu madhara ya magonjwa yasiyoambukiza, umuhimu wa kuchukua hatua za pamoja katika kuyazuia na kuyadhibiti

Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Chukua hatua dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza”ambayo inasisitiza wajibu wa kila mmoja wetu kufikia katika kuchukua hatua za kulinda afya yake na kusaidia jamii kuwa na maisha yenye ustawi

Magonjwa yasiyoambukiza ni Pamoja na saratani, kisukari, shinikiza la damu, magonjwa ya moyo, afya ya akili, figo, selimundu na baadhi ya magonjwa ya njia ya hewa. Takwimu za kidunia na za hapa nchini zinaonesha idadi ya wagonjwa kuongezeka, inakadiriwa kuwa zaidi ya asilimia 34 ya vifo nchini Tanzania vinatokana na magonjwa haya.

Kwa kuwa dalili za magonjwa haya huchelewa kutambuliwa na yanaweza kuzuilika, Wizara ya afya inawahimiza wananchi kufanya uchunguzi mara kwa mara ili kugundua magonjwa mapema na kuanza matibabu, kuzingatia mtindo bora wa maisha kwa kula mlo sahihi yenye virutubisho, kufanya mazoezi angalau dakika 30 kila siku, kuacha matumizi ya tumbaku na pombe na matibabu ya mapema ili kuzuia na kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza.

 


No comments