SERIKALI YAKABIDHI SIMBA SC KATIBA ILIYOBORESHWA KUENDELEA NA MCHAKATO WA MABADILIKO

 


Serikali imekabidhi uongozi wa klabu ya simba katiba mpya iliyofanyiwa maboresho na kuidhinishwa na Msajili wa vyama vay michezo kuwa inaweza kutumia katika uendeshaji wa klabu hiyo katika mfumo mpya wa hisa.

Akizungumza na waaandishi wa habari leo jijini Dar es salaa Msajili wa vyama vya Michezo Abel Ngilangwa amesema hatua iliyokuwa imebaki katika kuhitimisha rasmi mchakato huo ilikuwa ni kukabidhi kwa uongozi wa simba na kupokelewa kwa kusaini nyaraka za kukubali marekebisho jambo ambalo limekamilika na simba wamepokea.

Aidha ameweka wazi marekebisho ambayo yamefanywa katika katiba hiyo kuwa ni pamoja na kuweka tafsiri sahihi ya simba sports club campany limited ni kampuni iliyoanzishwa kisheria na itashughulikia shughuli za kibiashara na kiutendaji za klabu, umiliki wa hisa ukiwa wa ubia kati ya Baraza la Wadhamini kwa niaba ya wanachama na wawekezaji kwa mujibu wa sheria na maamuzi halali ya mkutano mkuu.

Pia kuweka bayana kuwa hisa za klabu zitamilikiwa kupitia baraza  la wadhamini kwaniaba ya wanachama, kuimarisha muundo wa Baraza la wadhamini lenye wajumbe watano na wasiozidi 7 watakao miliki na kusimamia mali za klabu kwa niaba ya wanachama.  

Kuweka wazi kuwa mkutano mkuu ndio chombo chenye mamlaka ya kuthibitisha Uteuzi na kumuondoa mjumbe wa Baraza la wadhamini pamoja na kuwa na muundo wa uwakilishi ndani ya Bodi kwa kuzingatia uwiano wa umiliki wa hisa kati ya wanachama na wawekezaji.

Ngilangwa amesema serikali imeidhinisha katiba hiyo kwa sababu maelezo hayo yanaendana na sheria ya baraza la michezo la Taifa, yanaimarisha utawala bora, uwazi na uwajibikaji pamoja na kuzingatia ushauri wa mwanasheria mkuu wa serikali aliyoutoa kwa klabu ya simba.

Vilevile maboresho hayo hayalengi kunufaisha watu wachache bali kuweka uwiano wa haki kwa wanachama na wawekezaji, kuondoa changamoto za kisheria na kiutawala na kuweka msingi thabiti wa usajili, umiliki na usimamizi wa mali kwa kuzingatia sheria za nchi.

Hata hivyo Ngilangwa amesema serikali inaamini kuwa kupitia katiba hiyo iliyoboreshwa klabu ya simba itajenga mazingira rafiki kwa uwekezaji, itaheshimu uwekezaji uliokwisha kufanyika na unaotarajiwa kufanyika hivyo kuepusha migogoro ambayo serikali haitarajii ijitokeze.

Amesisitiza kuwa sio jukumu la serikali kufanya uamuzi wa klabu kwenda kwenye aina nyingine ya uendeshaji bali kuidhidnisha marekebisho ya katiba yanayokidhi matakwa ya sheria na kwamba inajiridhisha kuwa marekebisho hayo hayaendi kuathiri maendeleo ya klabu, kuvuruga Amani miongoni mwa wanachama na kuvuruga usalama.

Ametoa wito kwa wanachama wa klabu ya simba na wadau wake wote kuhershimu maamuzi ya kisheria ili klabu kuendelea kuwa na utulivu mshikamano na mafanikio makubwa Zaidi










No comments