MILIONI 432 KUJENGA KITUO CHA TAALUMA EDWARD MPOGOLO DAR ES SALAAM.
HALIMASHAURI ya Jiji la Dar es Salaam, imetenga kiasi cha shilingi milioni 432, kujenga kituo cha umahili wa taalumu kitakachofahamika kwa jina Edward Jonas Mpogolo Center for Excellence Capacity Building.
Hayo yameelezwa katika hafla ya utangazaji matokeo ya mitihani ya ndani na utoaji wa tuzo kwa wanafunzi na shule za sekondari zilizofanya vizuri katika mitihani hiyo kwa kidato cha kwanza cha pil cha tatu na cha sita, jiji Dar es Salaam.
Aidha tuzo hizo zikitolewa kwa shule za sekondari zilizofanya vibaya kwa kukabidhiwa vinyago maalumu vya mpingo.
Akikabidhi tuzo hizo, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo, amesema, mkakati uliopo katika kuboresha sekta ya elimu ni kutekeleza Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050.
"Pia kutekeleza maono ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kuboresha miumdombinu ya elimu na ubora wa elimu itakayo mwezesha mhitimu kupata taaluma yenye tija," alisema Mpogolo.
Amesisitiza, Jiji la Dar es Salaam, linaendelea na ujenzi wa sekondari za ghorofa zenye vifaa vya kisasa,vitabu, kuimarisha nidhamu na uwajibikaji, matumizi ya teknolojia na kutekeleza mkakati wa kufuta ufaulu wa daraja sifuri na la nne.
Alipongeza halimashauri ya jiji hil kuamua kuwa na kituo cha taaluma alichosema kitakuwa ni chachu ya kuongeza ufaulu, kuwaongezea ujuzi walimu na kufanya tathimini ya elimu.





Post a Comment