BANDARI YA MTWARA NA SEKTA BINAFSI KUSHIRIKIANA KATIKA USAFIRISHAJI KOROSHO GHAFI

 


Bandari ya Mtwara imekusudia kushirikiana na sekta binafsi kuendesha Bandari Kavu lengo likiwa ni kufungasha kontena za Korosho ghafi zinazosafirishwa kupitia Bandari hiyo.

Meneja wa Bandari hiyo, Ferdinand Nyathi, amesema hayo wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Patrick Sawala, ya kukagua maeneo, shughuli na vifaa kwa ajili ya kuhudumia mizigo ya korosho kupitia Bandari ya Mtwara kwa msimu wa Korosho wa mwaka 2025/2026.

Mpango huo wa kushirikiana na sekta binafsi za Bandari ni kuhakikisha ufanisi mkubwa katika kuhudumia mzigo wa korosho.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Sawala, amesema lengo la uamuzi huo ni kuwahakikisha ufanisi wafanyabiashara na wasafirishaji kusafirisha mizigo yao kwa urahisi na kuendelea kutekelezwa agizo la serikali la kusafirisha korosho kupitia Bandari ya Mtwara.

No comments