TANZANIA KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI NA ALGERIA
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo ameafanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Algeria Mhe. Ahmed Attaf Jijini Cairo nchini Misri.
Mazungumzo hayo yamefanyika tarehe 19 Desemba, 2025 pembezoni mwa Mkutano wa Pili wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Afrika na Urusi
uliofanyika jijini Cairo, nchini Misri.
Katika kikao hicho, Mawaziri hao wamekubaliana kushirikiana kwenye masuala ya nishati, uwekezaji, pamoja na kuimairisha sekta ya utalii na kuanzisha safari za ndege kutoka Dar es Salaam kwenda nchini Algeria.
Pamoja na hayo, Mhe. Waziri Kombo amewakaribisha wawekezaji kutoka Algeria kuja kuwekeza nchini Tanzania kwenye sekta ya kilimo, ujenzi wa viwanda vya madawa, pamoja na kuanzisha tume ya pamoja ya masuala itakayosimiamia masuala ya uchumi baina ya nchi hizo mbili.
Katika kikao Viongozi wengine waliohudhuria ni Mhe. Paramagamba Kabudi, Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Balozi Ali Bujiku, na Balozi Noel Kaganda.

Post a Comment