PAPA KANISA KATOLIKI AVUNJA UKIMYA VITA MASHARIKI YA KATI
Kiongozi wa Kanisa Katoliki, Pope Leo, amesema leo Jumapili kuwa vifo na mateso yanayosababishwa na vita vinavyoendelea Mashariki ya Kati ni “fedheha dhidi ya binadamu”, huku akitoa wito wa kusitishwa mara moja kwa mapigano.
Akiwa anaongoza sala ya Angelus katika Uwanja wa Mtakatifu Petro, Vatican, Papa Leo alisema anaendelea kufuatilia kwa masikitiko makubwa hali ya vita inayoendelea Mashariki ya Kati na maeneo mengine yaliyoathiriwa na migogoro na vurugu.
Alisisitiza kuwa dunia haiwezi kunyamaza mbele ya mateso ya watu wengi wasiokuwa na hatia, akisema: “Hatuwezi kukaa kimya tunapoona mateso ya watu wengi, waathirika wasio na ulinzi wa migogoro hii. Kinachowaumiza wao kinaumiza ubinadamu wote.”
Papa Leo alitoa wito wa kuendelea na sala na juhudi za amani, akisisitiza umuhimu wa kusitisha mapigano ili kufungua njia ya kufikiwa kwa amani ya kudumu katika eneo hilo.

Post a Comment