NEMC YAKABIDHIWA CHETI NA MAKAMU WA RAIS BALOZI DKT.NCHIMBI


Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limekabidhiwa cheti na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Balozi Dkt.Emmanuel Nchimbi cha shukrani ya ushiriki katika sherehe za Usiku wa Muungano zenye kaulimbiu isemayo " Miaka 62 ya Muungano: Amani, Umoja na Mshikamano ni msingi wa maendeleo endelevu zilizofanyika katika ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Centre Jijini Dar es Salaam.


Akikabidhi cheti hicho, Dkt. Nchimbi alieleza umuhimu wa Taasisi mbalimbali za umma kushiriki kikamilifu katika shughuli za kitaifa zinazolenga kuimarisha umoja, mshikamano na maendeleo endelevu.


 Kwa upande wake, ushiriki wa NEMC katika hafla hiyo umeakisi dhamira ya Taasisi hiyo katika kuendeleza juhudi za kuunga mkono shughuli za Uhifadhi wa mazingira sambamba na kushirikiana na Serikali katika kutekeleza ajenda za kitaifa.








No comments