SIMBACHAWENE AKAGUA MASHAMBA YA MAGEREZA KAGERA
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe.George Simbachawene(Mb), Disemba 20, 2025 ametembelea Gereza Kitengule na kukagua shamba mkakati la kujitosheleza kwa chakula Magereza Mkoa Kagera pamoja na kuongea na maafisa na askari wa Gereza Kitengule.
Akikagua shamba hilo Mh.Simbachawene amesema Jeshi la Magereza linahitaji kuboresha mfumo wa uzalishaji mashambani kwa kutumia vifaa vya kisasa kwenye kilimo na kulima kilimo cha umwagiliaji ili kuepukana na changamoto ya hali ya hewa ambayo imekua ikiathiri uzalishaji kila mara.
"Ili kumrekebisha Mfungwa kwenye nyanja ya kilimo anapoingia Gerezani inahitajika mfungwa ajifunze kilimo cha kisasa kwa manufaa ya Jeshi pamoja na maisha yake baada ya kumaliza kifungo chake" alisema Simbachawene
Pamoja na hayo Mhe. Simbachawene aliongea na wafungwa na mahabusu wa Gereza Kitengule na kuwatia moyo kuwa gerezani siyo mahala pa mateso wala pakuondoa utu wao, bali ni sehemu ya kuwahifadhi na kuwarekebisha ili wanapomaliza kutumikia vifungo vyao wakawe raia bora na kuonesha yale waliyo jifunza wakiwa gerezani kwenye jamii.

Post a Comment