MRADI WA OPEC WAACHA TABASAMU KIJIJI CHA NGABOBO MKOANI ARUSHA
Zaidi ya
wananchi elfu 4 wa kijiji cha Ngabobo katika halmashauri ya Meru Mkoani Arusha
wamenufaika na mradi wa mfereji wa umwagiliaji Maji katika kijiji hicho.
Hayo
yamebainishwa na Afisa Kilimo wa Kata ya Ngabobo Godvoice Mbokoi, halmashauri ya Meru Mkoani
Arusha wakati akizungumza na waandishi wa habari kijijini hapo.
Mbokoi
amesema kuwa kupitia mradi huo wa Mfereji wa umwagiliaji umesaidia kuongeza
kipato kwa wakulima katika kijiji hicho kwani wakulima waliokuwa wakilima heka
moja awali sasa wanaweza kulima hadi heka tatu mpaka nne na kujiongezea kipato.
Ameongeza
kuwa mradi huo wa umwagiliaji umeondoa migogoro miongoni mwa wakulima wa kijiji
hicho .
Amesema
awali ilikuwa kuna malalamiko kwa baadhi wa Wakulima kutopata maji ila baada ya
mradi huo wakulima wote wamekuwa wakipata maji na kumwagilia mazao yao.
Mradi huo
wa Mfereji wa Umwagiliaji unatekelezwa
kupitia mradi wa Opec kupitia Mfuko wa Maendeleo ya jamii nchini Tasaf.
Mradi wa
Opec umefikia ukingoni Desemba 31 mwaka 2025


Post a Comment