WANANCHI WA KIJIJI CHA LAJA KARATU WAIPA KONGOLE TASAF
Wananchi wa kijiji cha Laja Wilayani Karatu Mkoani Arusha wameushukuru Mfuko wa Maendeleo ya jamii -TASAF kwa miradi waliyoitekeleza katika kijiji hicho.
Wananchi
hao wamezungumza hao kijijini hapo mbele ya waandishi wa habari na Mkurugenzi
Mtendaji wa Tasaf pamoja na baadhi ya watumishi wa mfuko huo.
Mkazi
mmoja wa kijiji hicho aliyejitamba kwa jina la Christina Lucas amesema Tasaf
kupitia mradi wa Opec imefanikisha ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Laja pamoja
na ujenzi wa madaraja katika kijiji hicho.
Amesema
Ujenzi wa Shule hiyo ya Sekondari Laja pamoja na mabweni umesaidia sana kuamsha ari ya elimu katika
kijiji hicho.
Ameongeza
kuwa awali wananfunzi katika kijiji hicho walilazimika kutembea umbali mrefu
kwenda na kurudi shule hali ambayo ilisababisha baadhi ya wanafunzi
kutohudhuria masomo vema kutokana na adha hiyo.
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Tasaf Shadrack Mziray amewataka wananchi wa
kijiji hicho kutunza miundombinu hiyo kwa manufaa ya kizazi kilichopo na
kijacho.



Post a Comment