WASHIRIKA WA MAREKANI KATIKA ENEO LA GHUBA WANAHUSIKA NA MASHAMBULIZI YA IRAN
Wizara
ya ulinzi ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) imesema hadi sasa
"imeshughulikia" makombora 165 ya balestiki, makombora mawili ya
baharini na ndege zisizo na rubani 541 za Iran.
Huko
Bahrain, Jumapili asubuhi uwanja wa ndege umeshambuliwa.
Haya
si matukio ya kawaida katika eneo hili, lakini tangu mzozo huu uanze Jumamosi
asubuhi, Iran inaonekana kupanua lengo lake kutoka kwa shabaha za kijeshi, kama
vile makao makuu ya Jeshi la Wanamaji la Marekani nchini Bahrain, hadi viwanja
vya ndege na maeneo mengine ya kiraia.
Sasa
hoteli za kifahari na maduka makubwa, majengo ya ghorofa ya juu, vituo vya juu vya
ndege vinaathirika mara kwa mara huku mapengo yakionekana katika ulinzi wa anga
wa mataifa ya Kiarabu katika Ghuba.
Maeneo
haya hayakuwahi kujengwa kwa matarajio akilini kwamba siku moja yatashambuliwa
na ndege zisizo na rubani na makombora ya balestiki.

Post a Comment